Vitunza taarifa kwenye kompyuta “storage devices”

 Vitunza taarifa kwenye kompyuta “storage devices”



Kompyuta ina aina mbili za memori

(a) “primary memory

Hii ni memori inayotunza taarifa kwa muda  mfupi ,

Unapozima kompyuta yako taarifa zilizo tunzwa kwenye memori hii “ram” hufutika moja kwa moja

Kwa mfano kama ulifungua programu ya “Microsoft office “ ukawa unaandika kitu , taarifa ya program hio inakua imetunzwa kwenye ramu, kama kompyuta yako itazima ghafla ina maana kila kitu ulicho andika kitafutika

Lakini kama ume tunza yaani ume “save” ina maana taarifa itaenda kwenye memori ya kutunzia documenti yaani “secondary storage”

ramu, inatunza taarifa za kompyuta pale tu unapokua umewasha kompyuta yako

(b) Seconday memory

Hii ni memori ya moja kwa moja

Hapa tunazungumzia “hard disk”

Kila kompyuta inaitaji sehemu ya kutunza taarifa kama vile picha , document na  mfumo endeshi wa kompyuta, kompyuta inahitaji sehemu ya kutunza taarifa hizi kwenye “storage drive”

Memori hizi hazifuti taarifa, zitaendelea kutunza taarifa hata kama utazima kompyuta


Kuna aina tofauti za memori hizi “internal storage drives”

Zinaweza kua "magnetic storage drive" , "solid state drive"

(a) Magnetic  hard drive

Hii ni memori ya ndani ya kompyuta iliyo undwa na disk zenye sumaku, ina 

Hii imegunduliwa mwaka 195

Imefunikwa kwenye kiboksi  kilichofungwa “sealed case” ,ndani yake ina disk zenye usumaku

Kwenye hizi disk ndipo ambapo taarifa “data” zinapotunzwa

Disk hizi huzunguka kwa spidi kubwa , na zinapozunguka ndipo ambapo mchakato wa kusoma taarifa “reading of data” na kutunzwa kwa taarifa yaani “writing of data” unapofanyika kwenye disk

Disk hutumia kebo  “SATA cable” ambayo hutumika kusafirisha taarifa kati ya hard disk na sehemu zingine za kompyta

(b)Solid state drive “haina sehemu inayo zunguka “

Hizi memori “drives” hazina sehemu zinazo zunguka

Hizi memori “drives” zinatumia chip ndogondogo za memori / vimemori vidogodogo, kama vile unavoviona kwenye flashi “flash momory chips” kutunza taarifa za kompyuta

Taarifa huweza kusafirishwa haraka sana

Kwa kua hazina sehemu zinazo zunguka , hazitoi sauti, na pia hazitumii umeme mwingi kwa sababu hio

SSD haziwezi kuharibika haraka kwa sababu ya mitikisiko au kuanguka kwa kua hazina sehemu zinazo zunguka zaidi ya 

SSD ni ghali zaidi

SSD zina ufanisi na spidi kubwa zaidi , ukitumia SSD inamaana spidi ya kompyuta yako itaongezeka


Matumizi ya SSD huongeza ufanisi na spidi kwenye kompyuta, unaweza kuongeza ramu , mpaka GB8 lakini kama “hard disk “ yako inakua ina spid ndogo usitegemee mabadiliko makubwa

Comments

Popular posts from this blog

KOZI YA KOMPYUTA KWA KISWAHILI

Lies the poor parent tell children