Acha kuongelea tu ndoto zako anza kuziishi

 Acha kuongelea tu ndoto zako anza kuziishi

Sielewi kile ninachotaka kufanya  sifanyi isipokua nisichotaka kukifanya, Hayo ni maneno ya mtume Paulo

Binadamu tuna tabia ya kufanya tusiyotaka kuyafanya na ku kushindwa kufanya tunachotakiwa kufanya

Kwa nini tunapenda kuongea tu na hatufanyi, kwa nini hakuna vitendo vya kusababisha mafanikio?,  Kwa nini tunafanya kile tusichopenda na kuogopa kufanya mambo ya msingi yanayoweza kubadili maisha yetu

Nitakueleza sababu tatu kwa nini unatamani tu kufikia ndoto zako lakini hufanikiwi kuzifikia, pia ninakueleza njia za kukuwezesha kuzifikia ndoto yako

#1 Maamuzi huleta maumivu

Kuna kipindi rafiki yangu alinilipia, nilikua nimefulia sana kiasi kwamba nilimuomba pesa ya kumwandalia  chakula na malazi, nilikua nikiishi nyumba ambayo haikua na umeme

Huyu rafiki aliekua akinitembelea alikua ni mtu ambaye tulikua tuna ndoto ya pamoja ya kutengeneza kampuni na kufanikiwa, pamoja na kweli kua nilikua kwenye biashara miaka nane bila mafanikio sikua na mafanikio yoyote, nlikua maskini sana miongoni mwa rafiki zangu waliokua na pesa

Nili teseka mda mrefu bila mafanikio

Tuna onta tuna tamani na tuna taka, lakini tuna epuka maamuzi kwa kua yanaleta maumivu

Maumivu huleta raha mwishoni, kwa mfano , kumbuka hadithi nliyokwambia, kuhusu mimi,  niliweza kufanikiwa baada ya mwaka tu baada ya rafiki yangu kuonana nami, ndani ya mwiezi michache tu nilikua Napata pesa nyingi kuliko wao, leo natengeneza pesa zaidi

Watu wanaovaha mataji leo ni wale waliobeba misalaba ajana

Watu wanaokula raha leo walivumilia maumivu jana

Binadamu tunataka kuepuka maumivu lakini maumivu huleta furaha baadae, usiogope maumivu

#2 hatuna uhakika kama tutafanikiwa

Hauna hakika kama ndoto zako zitafanikiwa

Binadamu ni mtu ambaye ana hofu ya vitu vitakavyo tokea

Mungu yu kwapi , je anapatikana wapi, 

Je nitafanikiwa kweli, hilo ni swali kila mtu hujiuliza na kushindwa kuchukua hatua

Ki ukweli hakuna uhakika kama utafanikiwa au huta fanikiwa

Watu wanaofanikiwa ni wale wanao tekeleza ndoto zao bila hofu, hata kama hawana uhakika watafanikiwa katika maisha yao

Nilipo anza ujasiriamali kila mmoja katika familia yangu alikua kinyume na mimi, watu wale walikua wana nipenda, na walijua hakuna hata mmoja katika familia yangu alie fanikiwa kufanya kile nilichotaka kufanya, hawakutaka ni feli,  vipi kama ninge feli,  hii ndio sababu walijalibu kunizuia ili nisiharibu maisha yangu

Lakini nilikua na ongozwa na dhamira kua umasikini ni hatari zaidi kuliko kifo

Nimekua katika sehemu ambapo umasikini ni mkubwa, najua umasikini nizaidi ya kifo

Kwahio nilipo anzisha kampuni japo sikua na uhakika,  Niliamua kuwa tajiri au kufa nikijaribu kutengeneza biashara

Unapotaka kufanikiwa kwa hamu kubwa kama unataka kupumua, utafanikiwa

Kama mafanikio yako ni muhimu sana kama oksijeni utapambana mpaka mwisho

#3 Tuna tamani kungekua na njia ya kimiujiza ya kufanikiwa

Binadamu tunapenda miujiza na utajiri wa haraka, kwa kua kuna sehemu yetu ambayo haiwez jua maisha ni rahisi na yanatakiwa kuwa rahisi

Hutaweza pata kirahisi, hata kama unaamini hivo, huwezi pata kirahisi mafanikio

Maisha ni magumu, Dunia ni uwanja wa mapambano, ni sehemu ya vita. Sijui kwa nini iko ivo,  lakini ndio uhalisia na siwezi kukuaminisha vinginevyo

Achana na kufikiria utajiri wa haraka, hakuna aliepata kwa urahisi, wote tuko kwenye jera moja, wote wanamatatizo na shida zao, inuka na upambane kupata unachotaka katika maisha

Acha kutegemea vitu vitakua rahisi

Pambana vita ya imani

Comments

Popular posts from this blog

KOZI YA KOMPYUTA KWA KISWAHILI

Lies the poor parent tell children